Saturday, April 28, 2012

BURUDANI YA LEO-DUNIA TUNAPITA

Tuburudike na Samba Mapangala dunia tunapita...

Thursday, April 26, 2012

WAPI USTAARABU WA MWANAMKE?

 

Zamani nilikuwa nahusisha kutokuwa mstaarabu inatokana na kutokuwa na elimu. Na kuwa wanawake wanaopenda kutumia lugha chafu ni wale ambao hawajasoma. Kumbe nilikuwa najidanganya; kwani siku hizi utaona matusi yanaandikwa mitandaoni mpaka unajiuliza hivi hawa wana akili timamu au wagonjwa? Kusema kweli sielewi kwanini watu tunagombana mitandaoni haswa wanawake na kuandikiana matusi ya nguoni. Tena basi wanawake haohao wanadai kuwa wao ni wasomi really? Msomi hatukani hovyo wala hana muda wa kuandika matusi mitandaoni...Tujirekebishe basi kidogo na kuacha ujinga huo!!!!!

KUNA UMUHIMU WOWOTE WA MUUNGANO?


 Kila April 26 ya mwaka tunasherehekea Muungano wa Tanganyika na Zanzibar chini ya hayati JK Nyerere na Abeid Aman Karume. Hivi bado tunauhitaji au ndo wakati umefika wa kuuachia? Wenzetu wazanzibari wanalia kila siku eti wanataka kuwa huru kutoka kwa "wadanganyika" wanavyodai kuwa wananyanyasika sana! Mhh mie sielewi wananyanyasika kivipi. Is it economically, socially or politically? Na kwanini sie watu wa bara tunang'ang'ania muungano? Kuna kitu chochote cha muhimu huko visiwani ambacho tunategemea sana kiasi ambacho tukivunja muungano tutaathirika? Mimi sioni manyanyaso yoyote tunayowapa wazanzibari kama wanavyodai wao. Ninachoona ni faida kubwa tu wanapata kupitia bara.

Charles Taylor guilty of aiding S. Leone war crimes






Liberian ex-leader Charles Taylor was convicted Thursday of arming rebels during Sierra Leone's civil war in return for blood diamonds, in an historic verdict for international justice.
In the first judgement against a former head of state by a world court since the World War II Nuremberg trials, Taylor was found guilty of 11 counts of war crimes and crimes against humanity by the Special Court for Sierra Leone.
"The trial chamber finds you guilty of aiding and abetting of all these crimes," said presiding judge Richard Lussick.
"The chamber finds beyond reasonable doubt that the accused is criminally responsible... for aiding and abetting in the commission of crimes one to 11 in the indictment," Lussick said at the court, based just outside The Hague.
Dressed in a dark suit, white shirt and red tie, the former president stood motionless as the verdict was read and showed no emotion afterwards.
He will be sentenced by the same court on May 30.
If sentenced to jail, Taylor will be held in a British prison.

Read more here:

Friday, April 20, 2012

RAIS ANAPOKWENDA BRAZIL KUKUTANA NA KOCHA...

Rais na mkewe wakisalimiana na  na Maximo kocha wa zamani wa timu ya taifa.
Alikuwa kapumzika kidogo tu baada ya misiba ya hapa na pale sasa huyo ameanza tena!! Kutumia fedha za wananchi kwenda nje na anachokifanya huko cha maana hakuna. Raisi wa nchi anatoka kwenda nje kukutana na kocha wa zamani wa timu ya taifa?? Au anawatanguliza waandishi wa habari (watu wake) Brazil na hao ndo waompokea huko kweli? Je hao waandishi wote wamelipiwa na makampuni yao au ni nani aliyewalipia? Ohhh nilisahau kuwa wengi wao ni wa magazeti ya serikali kwa hiyo ni pesa za serikali.



Rais akisalimiana na waandishi wa habari aliowatanguliza Brazil...


 Bado sijaelewa kama ilikuwa kuna umuhimu wowote wa kwenda Brazili na kukutana na kocha wa zamani wa timu ya taifa. Na kama kuna umuhimu raisi sio kazi yake ya kwenda nje na kutafuta kocha wa timu za Tanzania. Yeye ana majukumu nyeti sana sana kuliko ya kuwa kiguu na njia kila kukicha...Tumechoka na safari zake zisizo na mpango kwa taifa..Ana wawakilishi kila nchi kwanini asiwapeleke hao? Raisi sio lazima aende kila mahali au kila shughuli wakati ana watu wa ngazi za chini ambao wanaweza kumwakilisha yeye. Kama sivyo basi hakuna haja ya kuwa na mabalozi, mawaziri lukuki nk.

Tuesday, April 17, 2012

The Secret Service Prostitution Scandal Just Keeps Getting Bigger



 

 A preliminary investigation into the night of alleged debauchery involving members of President Obama's advance security team in Colombia has revealed that additional military personnel may have been involved in the prostitution scandal, Pentagon officials said Monday. 
The U.S. Southern Command initially reported that five members of the U.S. special forces had participated in the partying, but preliminary reviews of hotel security tapes indicate that the number was likely much higher. A senior defense official told the AP that "at least 10 military members may have been involved." 
Defense Secretary Leon Panetta said Monday that the agency is conducting a "full investigation" into the incident," and emphasized that he expects a strong response. 

Read more:http://articles.businessinsider.com/2012-04-16/politics/31348807_1_security-team-colombia-has-president-obama

BURUDANI-BIBI NAYE


Naona huyu bibi mwimbaji wa bongo flava alitaka aonekane kama kijana wa kisasa; akaamua kuweka haya mavazi. Waliomshauri hawakumshauri vizuri....

WAUAWA KWA IMANI ZA KISHIRIKINA

Wakazi wawili wa kijiji cha Kibande wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, Zegeli Shumba (60) na mkewe Bi. Helena Zengeli(58), waliuawa na kundi la watu wenye hasira kwa kupigwa mawe na miili yao kuchomwa moto kutokana na imani za kishirikina.
 
Kamanda Kashai amesema siku ya tukio hilo juzi majira ya saa 2.00 usiku kundi la wananchi wa kijiji hicho waliwavamia marehemu hao kwa kuwashambulia hadi kuwaua baada ya kutuhumiwa kuwa walikuwa wakijihusisha na vitendo vya kichawi.
 
Amesema kuwa hivi karibuni kulikua na binti mmoja kijiji hapo (hakumtaja jina) ambaye alipotea kwa njia za kutatanisha na marehemu hao walidai kuwa wangefanya maarifa ya kiganga kumrejesha lakini hadi wanauawa walikuwa hawajamrejesha jambo lililoibua hasira kwa wakazi hao

MWENYEKITI UVCCM ARUSHA AJIUNGA CHADEMA








MWENYEKITI wa UVCCM, Mkoa wa Arusha,kwa miaka mitano, James Ole Millya,ametangaza kujiuzulu nafasi zote kuanzia Taifa hadi Mkoa na kutangaza kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa madai kuwa CCM imefilisika kimawazo na haitoi matumaini kwa watanzania.

Aidha alisema hawezi kuendelea kupanda gari lenye pancha lukuki, hivyo ameamua kupanda gari lisilo na pancha na lenye kutoa matumaini mapya kwa watanzania.

Hayo ameyasema leo, wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye Hoteli ya Kibo Palace, iliyopo Jijini hapa. Amesema mara nyingi alikuwa akikemea mambo ambayo yanaweza kubomoa chama cha CCM kwa upendo, lakini alikuwa akipuuzwa kwa sababu ya chama hicho kuwa na kikundi cha wenyewe.

“Mimi nanukuu maneneo ya Nyerere kuwa alishawahi kusema CCM sio mama yangu na mimi pia CCM sio mama yangu na natangaza rasmi, kuondoka ndani ya chama hiki na najiunga na Chadema, sababu ndicho chama chenye kuleta tumaini jipya kwa watanzania,”alisema.

Ametaja nafasi alizoachia ngazi ni pamoja na Mjumbe kamati ya utekelezaji UVCCM Taifa, Mjumbe kamati ya siasa Mkoa na Mjumbe Halmashauri Kuu CCM Mkoa.

Amesema kuwa inasikitisha kuona Vijana wa UVCCM Mkoa wa Pwani, wanatoa matamko kuwa Rais ajaye 2015 hatatoka kanda ya Kaskazini na anayemfahamu ni Rais peke yake ambaye ni Jakaya Kikwete.
Millya alisema cha kusikitisha pale alipokemea kauli hiyo alipuuzwa na hadi sasa Ikulu haijawahi kutoa kemeo kwa Vijana hao na wala kukataza kauli hizo kutolewa, jambo lililompa jibu kuwa Ikulu inahusika kwa namna moja au nyingine na kauli hiyo.

Aidha alisema kuna Vijana wengi walioko ndani ya CCM wakiishi kwa  matumaini ya kusubiri kuteuliwa nafasi ya Mkuu wa Wilaya kama sio Mkoa, ila yeye hawezi kuishi kwa matumaini kama muathirika wa Ukimwi.
Hata hivyo alitoa wito kwa Vijana wote wenye nia ya dhati na mapenzi mema ya nchi yao, kumfuata Chadema ambako kunatoa tumaini jipya la maisha ya watu.

Millya ambaye alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa UVCCM tangu 2008 hadi sasa, aliwashukuru vijana  kwa kumpa ridhaa hiyo na ataendelea kuwashukuru, ila ameamua kwa ridhaa yake kuachia ngazi zote kwa ajili ya ukombozi wa kweli.
Millya hivi karibuni alijitosa kinyang’anyiro cha kugombea Ubunge wa Afrika Mashari ndani ya Chama chake cha CCM, lakini alichijiwa baharini na kutolewa jina lake.

Saturday, April 7, 2012

Tuesday, April 3, 2012

KWELI AKILI NI NYWELE....


UGOMVI WA BLOGGERS


 


 Nimemua kuzungumzia  hili tatizo la bloggers kutukanana katika blogs. Najua kuwa blogs ni ya mtu binafsi lakini sio kwa kutukana watu wengine. Hili jambo  linanikera sana. Imekuwa ni kawaida ya baadhi ya bloggers kutukanana/kugombana kwa mambo ya kijinga. Naita mambo ya kijinga kwasababu haiwezekani mtu kutomsifia mwingine ndio ilete ugomvi. Au kwakuwa sikutoa picha yako katika blog yangu basi ndio iwe tatizo. Mtu ameanzisha blog yake kwa hiyo ana amaamuzi ya kuandika vile anavyotaka yeye. Kama atamsifia mtu ni maamuzi yake yeye. Kwani kuna bloggers wengine ni "attention seekers" haitoshi kujiandika wenyewe wanataka na wengine nao wawe wanawaandika na kuwasifia. Wasipoandikwa basi ni matusi na kashifa zisizo na msingi... hebu tuelemike kidogo. Sio lazima jamani...kusifiwa kila siku. Tupendane  na kuheshimiana kama binadamu kwani tukiwa kama bloggers sie ni kioo cha jamii.

HONGERA CHADEMA-ARUMERU MASHARIKI



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEitDLon5DSCr-7O0PbGQ4YvAr4MM1taZaSYdkt1fRERPelDw4mt5_UmmmZt89R1swWqEQK-jX3WPfTzYUQAvAlYIGFYiVRHrnrv2hQYETJ-lcoblLtTYZvRbr-987rjm6n78txeqbvKqLyR/s640/the+two.jpg

Bw. Joshua Nassari wa CHADEMA


Sio siri wana ARUMERU wameonyesha kuwa hawacheki na mafisadi..na wala hawababaishwi na ahadi za kijinga. Mara nyingi tumeona katika uchaguzi mbalimbali ambapo CCM huwaonga wananchi wake kwa chakula na ahadi zisizo kamilika. Ushindi wa Mh. Nassari unainyesha ushupavu wa wananchi wa kuonyesha kuchoka kuongozwa na viongozi wabovu wasiojua mwelekeo. Hawakutaka kufuata mambo ya kuongozwa na warithi; wao wanachjua ni Demokrasia ya kweli.
Kwa Mujibu wa Matokeo hayo mgombea ubunge wa Joshua Nassari CHADEMA amepata kura 32,972, na kumshinda Mgombea mpinzani wake mkuu katika uchaguzi huo, Sioi Sumari wa Chama cha Mapinduzi (CCM) aliyepata kura 26,757.Kwamatokeo hayo inafanya kuwa idadi ya Kura zilizompa ushindi Nassari wa Chadema kuwa kura 6,215 dhidi ya Sioi Sumari CCM.