Zamani nilikuwa nahusisha kutokuwa mstaarabu inatokana na kutokuwa na elimu. Na kuwa wanawake wanaopenda kutumia lugha chafu ni wale ambao hawajasoma. Kumbe nilikuwa najidanganya; kwani siku hizi utaona matusi yanaandikwa mitandaoni mpaka unajiuliza hivi hawa wana akili timamu au wagonjwa? Kusema kweli sielewi kwanini watu tunagombana mitandaoni haswa wanawake na kuandikiana matusi ya nguoni. Tena basi wanawake haohao wanadai kuwa wao ni wasomi really? Msomi hatukani hovyo wala hana muda wa kuandika matusi mitandaoni...Tujirekebishe basi kidogo na kuacha ujinga huo!!!!!
No comments:
Post a Comment