Wakazi
wawili wa kijiji cha Kibande wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, Zegeli
Shumba (60) na mkewe Bi. Helena Zengeli(58), waliuawa na kundi la
watu wenye hasira kwa kupigwa mawe na miili yao kuchomwa moto
kutokana na imani za kishirikina.
Kamanda
Kashai amesema siku ya tukio hilo juzi majira ya saa 2.00 usiku kundi
la wananchi wa kijiji hicho waliwavamia marehemu hao kwa
kuwashambulia hadi kuwaua baada ya kutuhumiwa kuwa walikuwa
wakijihusisha na vitendo vya kichawi.
Amesema kuwa
hivi karibuni kulikua na binti mmoja kijiji hapo (hakumtaja jina)
ambaye alipotea kwa njia za kutatanisha na marehemu hao walidai kuwa
wangefanya maarifa ya kiganga kumrejesha lakini hadi wanauawa
walikuwa hawajamrejesha jambo lililoibua hasira kwa wakazi hao
No comments:
Post a Comment