HAWA NDIO WANAPASWA HASA KUFUNGWA MAISHA AU KUNYONGWA KABISA. NIKIWA KAMA MWANAMKE NA MAMA; KUSEMA KWELI NALAANI VIKALI WATU AMBAO WANAWAFANYIA UKATILI WATOTO WADOGO. HII SI MARA YA KWANZA KUSIKIA MATUKIO KAMA HAYA YA WATU KUWACHOMA WATOTO MOTO. LAKINI JE WATU HAWA WANAPEWA ADHABU GANI? INATAKIWA WAPEWE ADHABU AMBAYO WENGINE WASITENDE UNYAMA HUO KABISA!!!
 |
Mtoto huyu (3) amechomwa moto na shangazi yake ni ukatili gani huu... |
|
|
|
|
|
Mtoto huyu akiwa hospitali baada ya wasamaria wema; akiwa hospitali ambapo madaktari wamemfanyia upasuaji na kuondoa mkono uliothirika kwa moto!
Mwanamke ambaye anadaiwa kumchoma moto mtoto huyo wa miaka 3. Huyu ni shangazi wa mtoto huyo kweli?? Ana rorho gani ya kuweza kufanya unyama huo??
Na Elly Mbeyale
HALI ya Mtoto Aneth Johanes (4) aliyelazwa katika Hospitali ya Rufaa
ya Mbeya kufuatia kuchomwa moto mkono wake wa kushoto na anayedaiwa kuwa
ni Shangazi yake inaendelea vizuri licha ya kufanyiwa upasuaji
uliolazimu kukatwa kwa mkono huo.
Kwa mujibu wa mama mdogo wa mgonjwa anayemhudumia hospitalini hapo
Silvia Salvatory alithibitisha kuendelea vizuri kwa motto huyo ambapo
alisema ilimlazimu kufanyiwa upasuaji kutokana na mkono huo kukosa
mawasiliano na kuonekana kuvunjika.
Alisema taarifa za awali zinaonesha shangazi yake huyo Bahati Rukangara
alianza kumtesa mtoto huyo muda mrefu mara baada ya kumchukua kutoka kwa
wazazi wake wanaoishi Bukoba Mkoani Kagera.
Aliongeza kuwa tangu amchukue kwa wazazi wake Februari Mwaka huu
amewahi kumjeruhi mkono wake wa Kulia hadi kuuvunja ambapo hadi sasa
mtoto huyo alikuwa akitegemea mkono wa kushoto ambao umekatwa.
Tukio hilo la kisikitisha lilitokea juzi majira ya saa nne asubuhi
baada ya majirani kusikia yowe la mtoto huyo akiomba msaada kutokana na
mateso na maumivu makali aliyokuwa akiyapata kutokana na adhabu hiyo
kutoka kwa Shangazi yake
Muuguzi mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya Thomas Isidori alisema
hali iliyopelekea kukatwa kwa mkono wa mtoto huyo ni siri kati yake na
daktari aliyemhudumia na kwamba sheria ya uuguzi inakataza kutoa taarifa
ambazo ni siri.
Isidori alipoulizwa sababu za mgonjwa huyo kufanyiwa upasuaji mapema
mno hadi kusababisha ulemavu alisema ni suala la kitaalamu ambalo hata
yeye hawezi kulijibu na ni sheria ambayo inawataka madaktari kutunza
siri za wagonjwa.
Hata hivyo muuguzi huyo alizuia kabisa waandishi wa habari kupiga
picha za motto huyo baada ya kufanyiwa upasuaji huo uliosababisha
kukatwa mkono kwa mgonjwa huyo.
Baadhi ya wananchi waliofika Hospitalini hapo kumjulia hali mtoto
Aneth aliyelazwa Wodi namba Nane ambao hawakutaka kutaja majina yao
walilaani kitendo cha madaktari kukimbilia kukata mkono mgonjwa badala
ya kujaribu njia zingine za kunusuru hali hiyo.
SOURCE: sundayshomari.com