Friday, November 16, 2012

WASANII WA KIBONGO KWA KUIGA....

Wabongo hivi hatuwezi kuanzisha kitu wenyewe bila ya kuiga? Tukiangalia MOVIES nyingi za kibongo maudhui mengi yamekaa "kinigeria" hadi kuongea kwa "kupayuka". Tujaribu basi hata kufanya vitu wenyewe basi...manake tumewaiga wazungu sana tu tukaona hapana sasa hata "wapopo" nao?
Tukija upande wa Music ndo usiseme yaani watu wana copy & paste bila hata aibu! Tushukuru kuwa nchi yetu haijulikani otherwise tungekuwa tunashtakiwa kwa mambo ya "copyright infringement". Kila siku Baraza la sanaa na wasanii wenyewe huwa wanalalamika kuwa wanaibiwa kazi  zao! Sasa na wao mbona wanaiba kazi za wenzao?

Angalia huu wimbo wa OLIVER TWIST wa D'banji  then angalia msanii LINAH wa Tanzania alivyocopy!!






Linah Oliver Twist

No comments:

Post a Comment