Sunday, August 19, 2012
EID MUBARAK TO ALL MUSLIMS!
SEMA SIKIKA BLOG WOULD LIKE TO WISH ALL MUSLIMS AROUND THE WORLD EID MUBARAK!
Wednesday, August 15, 2012
TANZANIA OLYMPIC YALE YALE....Kichwa cha mwendawazimu!
Tanzania siku zote ni wasindikizaji tu kwa kitu; tunajaribu kila fani ila tunakuwa washika mkia tu. Kwenye fani ya urembo ni wa mwisho, mpira ndio usiseme yaani kwa ujumla michezo sisi ni zero! Mbona wenzetu Wakenya wanaweza? Waganda wanajaribu ila sisi tunashindwa nini? Haiwezekani unawapeleka watu walewale ambao walishindwa miaka iliyopita au ndo kujuana? Unajua kabisa mtu alichemka kipindi kilichopita then unamchukua yule yule. Mie ninahisi kuna walakini katika kuchagua wawakilishi wa mashindano ya nje "olympic". Wenzetu wanachukua miaka kujitayarisha sie tunasubiri mwezi sijui au week. halafu basi wanaondoka na "maafisa" kibao wote wa nini? Ni kupoteza tu pesa za wananchi. Ni bora kutokuwa na wawakilishi kuliko kupeleka watu ambao hawafanyi vizuri hata hawajaribu kabisa!!
Dr Ulimboka Arejea nchini
Kuna usemi kuwa Mungu si Athuman ambao unamaanisha kuwa uwezo wake haufananishwi na binadamu yoyote. Ni pale anavyoamua yeye jambo litokee linatokea lakini asipoamua yeye hakuna anayeweza kupanga wala kupangua. Je kuna mtu yeyote alidhani kuwa Dr ulimboka atatembea tena?
Mwenyekiti wa jumuia ya madaktari Tanzania Dr Steven Ulimboka aliyekuwa nchini Afrika ya kusini kwa ajili ya matibabu baada ya Kutekwa kupigwa na "watu wasiojulikana" amerejea nchini na kulakiwa na madaktari wenzake,wanaharakati wa haki za binadamu na wananchi wa kawaida. Je haki itandeka kwa wale waliomfanyia unyama kwa kufikishwa mahakamani? Au hata wakifikishwa mahakamani hukumu yao itakuwa vipi au ndio itakuwa kama kawaida yao ya "kuwaachia kwa dhamana". Au kuwa hakuna ushahidi wa kutosha au uchunguzi unaendelea...na tume imeshawekwa kufanya uchunguzi huo..
Subscribe to:
Posts (Atom)