 |
Dr. Steven Ulimboka kabla ya kipigo |
 |
Hapa baada ya kupigwa. |
Kiongozi wa mgomo wa madaktari
Bw. Steven Ulimboka ameokotwa maeneo ya Mabwepande akiwa amepigwa
mapanga na hali yake ikiwa ni mbaya Fullshangwe imepata habari kuwa
kulikuwa na gari lililokuwa likipeleka katika hospitali ya TMJ Mikochezi
na lilipofika hapo walimhamishia kwenye Ambulance na kumuwahisha
hospitali ya Muhimbili kitengo cha mifupa Moi kwa matibabu.
Kamanda
wa polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamanda Suleiman Kova
akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio la utekaji nyara na
kujeruhi lililompata kiongozi mgomo wa Madaktari Steven Ulimboka
anayedaiwa kutekwa na watu watano wakati akipata kinywaji katika klabu ya
Leaders Kiondoni jijini Dar es salaam.
Kamanda Kova amesema Ulimboka aliokotwa na msamaria mwema ambaye
hakutaka kumtaja jina lake kiusalama na kutoharibu upelelezo kuwa
msamaria mwema huyo alimuokota Ulimboka katika msitu wa Mabwepande na
kutoa taarifa kituo cha polisi cha Bunju, ambapo polisi aliyekuwa zamu
alichukua maelezo yake na baadae Steven Ulimboka kuletwa katika
hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Kamanda Kova amesema jeshi la Polisi Kanda Maalum limeunda jopo maalum
kwa ajili ya uchunguzi na upelelezi wa tukio hilo la utekaji nyara,
kwani ni tukio la kwanza kutoke nchini, ameongeza kwamba wahusika wote
watakaobainika kuhusika na tukio hilo wachukuliwa hatua za kisheria na
sheria itafuata mkondo wake ili kukomesha matukio mengine kama hayo.
SOURCE:FULL SHANGWE BLOG
No comments:
Post a Comment