Sunday, May 27, 2012

ZANZIBAR NINI TENA?

Sheikh Farid Hadi Ahmed akiongoza maandamano "ya amani".

Kikosi cha kutuliza fujo (FFU) kikiwa tayari kuwadhibiti waandamanaji ambao wanadaiwa kuandamana bila ya kibali



Kanisa ambalo linadaiwa kuchomwa na wazanzibar waliofanya maandamano.
Maelfu ya wazanzibariwamefanya maandamano amani kuishindikiza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuitisha kura ya maoni juu ya Muungano na kupeleka ujumbe kwa Umoja wa Mataifa wa kutaka Zanzibar kujitenga kama ilivyofanya Sudan ya Kusini.
Wazanzibari hao wakiongozwa na Sheikh Farid Hadi Ahmed walitembea kutoka viwanja vya Lumumba na kupitia barabara ya Kinazini, Mpigaduri, Michenzani Maskani ya CCM Kisonge, kwa Biziredi na kurudi tena viwanja vya Lumumba.
Maandamano hayo walioyaita matembezi ya amani yalifanyika na kuhudhuriwa na maelfu ya wazanzibari ambapo awali kuliandaliwa kongamano kubwa lililoandaliwa na Taasisi za Kiislamu kwa kushirikiana na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) kwa lengo la kuzungumzia mfumo wa elimu Zanzibar.
SOMA ZAIDI:

No comments:

Post a Comment