Dr Mwakyembe roho nyeupe...unafiki mtupu!!!
Naona sasa Dr. Mwakyembe roho nyeupe baada ya kuzawadiwa "ulaji" na mkuu wa ulaji au mkuu wa kaya. Kuteuliwa kwa Mwakyembe kuwa waziri wa uchukuzi naona ni njia mojawapo ya kumshukuru kwa kumfichia siri mkuu wa kaya. Nakumbuka alikuwa anaahidi kufichua siri kila kukicha lakini ghafla alikaa kimya. Mhh kumbe alikuwa anasubiria akijua atapatiwa something na mkuu wa kaya. Huu ni unafiki mtupu wa viongozi wetu kucha ni kufichiana maovu na kutufanya sisi wananchi wapumbavu.Kwahiyo inaonyesha kabisa yale yote aliyokuwa akiyasema yalikuwa ni dangya toto. Na kuwa yeye na wengine wote aliokuwa akiwashutumu ni walewale. Wote wapo pamoja katika kula pesa za watanganyika.
No comments:
Post a Comment