Saturday, October 8, 2011

Wanawake Tupendane...

 





Hivi kwanini wanawake hatupendani? Utakuta watu ni marafiki wakubwa, wanashare everything lakini  wakiwa na watu wengine wanasemana. Kuoneana wivu wa kijinga ambao hauna hata msingi. Imefikia kukuta usemi huu "mwanamke umbea kusutwa suna". Kwanini basi tusifanye mambo ya maendeleo kuliko kuchunguzana, kusemana na kugombana? Imefikia wengine wanatolena siri zao FACEBOOK na kutukanana matusi ya nguoni na huku wengine wakishangilia...Pia wanatoleana siri za ndani nikikuambia mambo yangu ujue kuwa nakuamini sasa inakuwa vipi unawaambia watu wengine? Wengine wanafikia kutishiaana kupigana! Hivi karne hii ya leo watu wanapigana kweli? Mie nadhani tushindane kwa kufanya vitu vya maendeleo.. 
 
Tena basi hao wanaotoa matusi wanadai kuwa ni wasomi, really? Wasomi hawana muda wa kuangalia mambo madogo madogo na ugomvi wa kijinga. Kama wewe ni tajiri na mwengine ni maskini haijalishi umetoa wapi utajiri wako. Kwanza matajiri hawajigambi wapo kimya na mali zao sasa sisi wakina "kapuku" kutwa maneno.

Hii tabia ni mbaya sana wanawake wenzangu tafadhali tupendane na tusitiriane jamani...
Burudika na mwanamziki Demarco "TRUE FRIEND"



No comments:

Post a Comment