Thursday, October 13, 2011

MWALIMU NYERERE 1922-1999

Mwl. JK NYERERE  1922-1999

 Ikiwa ni miaka 12 tangu Raisi wa kwanza wa jamhuri ya Tanganyika na baadaye Tanzania aage dunia, watanzania bado tunamkumbuka. Alikjulikana kama mwalimu ambaye alikuwa mwalimu kweli na si wa vyeo vya kujipachika. Watanzania inatupasa tumkumbuke kwa mazuri aliyotenda; mtu wa watu aliyependa watu, mchapa kazi na mtetea  haki za wanyonge. Alitetea haki si Tanzania tu bali Afrika kwa ujumla...









Alipozungumzia kilimo au kufanya kazi kwa bidii alionyesha kwa vitendo. Kwani alikuwa akijua utawala bora ni kitu gani; na yeye kama kiongozi alikuwa mstari wa mbele kuonesha mfano.

 
Ujamaa hatukuuona umuhimu wake lakini sasa tunakumbuka yote aliyoyafanya katika kipindi chake. Tulikuwa na umeme hakukukuwa na mgao wa kijinga kama huu uliopo chini ya uongozi wa Kikwete. Alikuwa ni kiona mbali haswa kuhusu uongozi/kuchagua viongozi ndani ya CCM. Alijua  nani ni kiongozi na yupi mbabaishaji. Je hatuoni yale aliyokuwa akisema yametokea?


Aliamini kuwa maendeleo ya nchi siku zote hupatikana kwa kuwahusisha wananchi wenyewe."If real development is to take place, the people have to be involved."
Julius Kambarage Nyerere, from his book Uhuru na Maendeleo (Freedom and Development), 1973.


UTAKUMBUKWA DAIMA... REST IN PEACE.....

1 comment:

  1. Tutakukumbuka daima baba wa Taifa..mwenyezi Mungu akulaze pema peponi

    ReplyDelete