Friday, July 20, 2012

RAMADHAN NJEMA

Wishing all Muslims around the World Ramadhan Mubarak!!!



Wednesday, July 18, 2012

AJALI YA MELI ZANZIBAR!!!!!

Moja ya maiti iliyoopolewa baada ya ajali


Majeruhi 


 

Meli iliyokuwa imewabeba takriban watu miambili imethibitiswha kuzama katika bahari ya hindi eneo la Chumbe kisiwani Zanzibar. Meli hiyo kwa jina Star Gate ilikuwa inatoka Dar Es Salam kuelekea Zanzibar.
Kulingana na taarifa za vikosi vya wanamaji , meli hilyo ilianza kupata matatizo baada ya kutokea mawimbi makali.
Jeshi la polisi la wanamaji nchini Tanzania limeanza shughuli za kuwaokoa watu zaidi ya mbia mbili wanaohofiwa kuwa kwenye meli ya Skagit inayoripotiwa kuzama huko visiwani Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa za polisi, ingawa hawajathibitisha idadi kamili ya abiria waliomo kwenye meli hiyo, lakini wamethibitisha kwamba meli hiyo imepigwa na dharuba ya upepo mkali katika eneo la Chumbe pindi ilipokuwa inatoka jijini Dar es Salaam kuelekea visiwani Zanzibar.
Itakumbukwa kwamba, ni takriban mwaka mmoja sasa tokea ajali ya meli iliyokuwa imezidisha mizigo kuzama katika pwani ya kisiwa cha Zanzibar ikiwa na watu takriban 800.
Mwandishi wa BBC mjini Dar Es Salam, Aboubakar Famau anasema kuwa meli hiyo MV Skagit ilianza kuzama saa sita saa za afrika mashariki ikiwa inaelekea bara.
Safari kati ya bara na pwani huchukua saa mbili. Inaarifiwa huenda watoto thelathini na moja walikuwa kwenye meli hiyo.
Afisaa wa usalama katika bandari ya Zanzibar alifahamisha shirika la habari la Reuters kuwa meli hiyo sasa imebiruka.
"maiti kumi na wawili pamoja na manusura kumi tayari wameodolewa baharini kufikia sasa.
Shughuli za uokozi zinaendelea ingawa kuna changamoto ya hali mbaya ya hewa." hii ni kwa mujibu wa waziri katika ofisi ya rais Mwinyihaji Makame,
Kivukio kilichoko kati ya Dar es Salaam na Zanzibar huwa na shughuli nyingi sana na huvutiwa sana na watalii pamoja na wenyeji wa Tanzania.

Habari pamoja na picha kutoka BBC

Nelson Mandela Birthday: Millions Of South African Children Sing For Loved Leader





JOHANNESBURG — Nearly 12 million children across South Africa kicked off celebrations Wednesday for the 94th birthday of Nelson Mandela, the country's deeply loved anti-apartheid icon, with resounding choruses of Happy Birthday.
Mandela is expected to spend the day privately with his family at their homestead in his southeastern birth village of Qunu. Meanwhile, communities in South Africa and around the world were dedicating 67 minutes of the day to volunteer work and projects for the needy – one minute to mark each of Mandela's 67 years in public service.
Mandela became South Africa's first black president in 1994 after spending 27 years in prison for his fight against racist apartheid rule, and was awarded a Nobel Peace Prize for his efforts.
Tributes to Mandela poured in early Wednesday, with U.S. President Barack Obama saying Mandela "has changed the arc of history, transforming his country, the continent and the world."
Ahmed Kathrada, one of Mandela's oldest friends, said Madiba, as he is affectionately known by his Xhosa clan name, championed the dignity of all.
`'You can be rich but if you don't have dignity you are a second-class citizen," Kathrada said in a public lecture marking the birthday celebrations.
Tokyo Sexwale, a longtime ally in the governing African Nation Congress, described Mandela as a global statesman who inspired the world.
At one Johannesburg elementary school Wednesday, children watched a film documenting Mandela's life and his years of service and sacrifice along with a photographic display of him meeting celebrities including Beyonce, Michael Jackson and Cristiano Ronaldo.
"Nelson Mandela set an example to show us that reconciliation is possible," said 10-year-old Thakgalo Ditabe. She said she wanted Mandela to know how much he meant to her.
Ntando Ntuli, 12, said with pride: "He is my hero because he fought for us. He is an icon, the king of Africa."
In 2009, the United Nations established Nelson Mandela International Day to honor the African leader on his birthday through acts of community service.
In many districts, South Africa came to a virtual standstill early Wednesday as strangers greeted each other in the streets and even infants at one pre-school waved at passersby and sang: "We love you, Tata," or `'great father," a supreme term of endearment.
In the eastern port city of Durban Sir Alex Ferguson, manager of England's Manchester United football team that is widely followed in Africa, sang Happy Birthday over a cake iced with the image of the team's yellow and red badge.
http://www.huffingtonpost.com/2012/07/18/nelson-mandela-birthday_n_1682171.html

Tuesday, July 17, 2012

Wanafunzi kupokea wageni kutoka nje


Hakuna jambo lililokuwa linanikera kama kuambiwa kujipanga barabarani kupokea viongozi wandani au wa nje. Hivi hawa viongozi huwa wanafikiria nini kuwachukua wanafunzi mashuleni kwenda kujipanga barabarani kupokea viongozi? Wana Hawajui kuwa watoto wanapoteza muda wa masomo yao. Wanajifanya wanawajali wanapowahitaji tu badala ya kuboresha elimu yao. Sasa hii ya kuwachukua na kuwapeleka IKULU kabisa eti kumpkea raisi hii kali!!

Tuesday, July 10, 2012

BIG UP SOLO THANG!

NAONA KUNA WASANII WACHACHE SANA WENYE UCHUNGU NA NCHI YAO...NA SIO WALE WANAONUNULIWA WAKATI WA  UCHAGUZI KUPIGIA DEBE VYAMA VYA KISIASA NCHINI. MSIKILIZE SOLO THANG NA WIMBO WAKE "MISS TANZANIA" ANAVYOELEZEA VIONGOZI WA NCHI YETU WALIVYOOZA NA KUNUKA KWA MATENDO YAO!!!!


Sunday, July 8, 2012

KILA LA HERI TIMU YA OLYMPIKI TZ





Timy ya taifa ya Tanzania inayowakilisha mashindano ya olympic London.
LABDA MWAKA HUU WATAONDOA ILE DHANA YA KUWA WASINDIKIZAJI KAMA KAWAIDA YETU KATIKA KILA FANI.TUAWATAKIA KILA LA HERI KATIKA KUWAKILISHA NCHI KWEYE MASHINDANO YA OLYMPIKI!!

HUYU NDIO ANAYEDAIWA KUMTEKA DR. ULIMBOKA

Polisi ACP Msangi




ASKARI anayetuhumiwa kumteka Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka, Kamishna wa Polisi Msaidizi (ACP), Ahmed Msangi, amehojiwa na kuzungumzia kilichotokea kuhusiana na tuhuma kwamba aliambiwa arejeshe simu ya mkononi na pochi ya Dk. Ulimboka.
Akizungumza na Gazeti la JAMHURI, ACP Msangi alikiri kwenda katika wodi ya wagonjwa mahututi katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa nia ya kumhoji Dk. Ulimboka, ila akaeleza mshangao wake kutokana na habari zilizochapishwa mwishoni mwa wiki, kuwa aliambiwa arejeshe pochi na simu ya Dk Ulimboka kwa maana kuwa alivipora walipomteka.
Vyombo vya habari mwishoni mwa wiki vilichapisha taarifa bila kutaja jina la askari anayetuhumiwa, lakini pia ukawa unasambazwa ujumbe mfupi kupitia simu za mkononi ambao ulisema hivi:
“Kamanda Msangi aliyemkamata na kumtesa Dr. Ulimboka, yuko katika jopo la kuchunguza nini kilimtokea Dk. Ulimboka. Alipofika kumhoji Dk. Ulimboka alimwambia ‘Nirudishie simu na wallet yangu’. Kamanda Msangi taratibu akaondoka wodini kichwa chini. Kama wewe ni mpenda haki na unapinga ujinga na dhuluma, watumie ujumbe huu watu wengi kadri uwezavyo ili wamjue dhalimu aliyeongoza unyama huu,” ulisema ujumbe huo unaosambazwa kupitia simu za mkononi.
Tume ya Jeshi la Polisi iliyoundwa kuchunguza tukio la Dk. Ulimboka kutekwa nyara, kwa mujibu wa Kamanda Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, inaongozwa na Kamanda Msangi.
 Kamanda Msangi (pichani)azungumza
Jamhuri: Afande umetangazwa kuongoza hii Tume ya Polisi kuchunguza suala la Dk. Ulimboka, lakini taarifa zilisosambaa zinaonyesha Ulimboka alikwambia umerejeshee simu na wallet yake. Unalizungumziaje hili?
Kamanda Msangi: Hata mimi nimesikia hizi taarifa, na zimenisikitisha mno. Naamini taarifa hizi zina malengo ya ziada. Si kweli kwamba nilishiriki kumteka Dk. Ulimboka na wala sijawahi kuwa na wazo hilo.
Jamhuri: Ikiwa hukushiriki kumteka iweje wodini akwambie nirudishie simu yangu?
Msangi: Kwanza ifahamike mimi huyu Dk. Ulimboka na mwenzake Dk. Deo nimewafahamu siku nyingi sana. Kwa maana hiyo ni mtu anayenifahamu vizuri tu. Kuna upotoshaji wa makusudi umefanywa ambao mimi nadhani una msukumo wa kisiasa.
Alichosema Dk. Ulimboka nilipozungumza naye, ni kwamba simu moja ilidondoka, nyingine wale watu waliomteka wameichukua pamoja na wallet yake. Hivyo alikuwa ananitajia vitu vilivyopotea. Nilipomuuliza iwapo anakumbuka namba ya simu, aliniambia nikamuulize Dk. Deo. Sasa nashangaa mtu aliyepenyeza uongo huu kwamba alisema mimi ndiye niliyempora hivyo vitu… sielewi ni nani na ana malengo gani.
Jamhuri: Haya unayasema wewe, hivi unadhani jamii itakuamini kwa kauli hizi, haitaonekana unajitetea tu?
Msangi: Wakati anazungumza maneno haya, alikuwapo Profesa Museru ambaye ni Mkurugenzi wa MOI. Sina cha kuficha kamuulize tu, atakwambia alichosema Dk. Ulimboka. Yupo pia Dk. Deo, huyu ananifahamu na Dk. Ulimboka anasema walikuwa wote wakati anatekwa. Dk. Deo ananifahamu, akaulizwe iwapo mimi ndiye niliyemteka Dk. Ulimboka.
Jamhuri: Tuhuma hizi zilianza kusambaa mapema tu Ijumaa. Je, wewe hukuwa na hofu kwenda pale MOI kumhoji Dk. Ulimboka?
Msangi: Ndugu yangu, nchi hii ina askari wengi mno. Hivi mimi kwa akili ya kawaida naweza kushiriki kumteka Dk. Ulimboka kisha nikaenda wodini kumhoji? Hata katika akili ya kawaida ya binadamu hilo haliwezekani.

Jamhuri:
Hizi tuhuma zilizoelekezwa kwako ni nzito. Wewe ndiye uliyeteuliwa kuongoza Tume ya Uchunguzi wa tatizo hili. Je, unadhani uchunguzi utakaofanya utaaminiwa na wananchi ukitoa ripoti?
Msangi: Mimi ninachokuhakikishia sikushiriki kumteka na si kweli kwa kila hali. Mambo kama haya yanakatisha tamaa. Kama tunaanza kuzushiana uongo kwa kiwango hiki, nchi hii sijui inaelekea wapi! Kimsingi imenikatisha tamaa mno. Wapo wanaosema nijiuzulu katika Tume hii lakini mimi nasema wakubwa wangu wamenipa kazi hii na watakaloamua nitalipokea.
Hivi wewe gazeti lako likituhumiwa unaacha kuendelea kutafuta habari? Nitaendelea kufanya kazi hii kama nilivyoapa siku nilipohitimu mafunzo kwamba nitalitumikia taifa kwa uadilifu na uaminifu wa hali ya juu katika kiapo changu cha utii. Na hilo ndilo nitakaloendelea kufanya. Watu wanapenda kuharibiana maisha tu.
Profesa Museru asema alichokisikia

Habari hizi zimechapishwa na Gazeti la Jamhuri

Saturday, July 7, 2012

Burudani ya leo-SHOUT FOR FREEDOM

DR Ulimboka azumgumza

Hebu sikilizeni wenyewe jamani hivi nchi hii inaenda wapi?