Najua kuzungumzia huruma hii inajulikana wazi kuwa KIKWETE NA BARAZA LAKE hawana huruma kabisa na wananchi wao! Haiwezekani watu umeme mmewakatia, huduma za jamii ni mbaya kuliko. Huduma ya afya ndo usiseme...madaktari wetu wanajitahidi hivyo hivyo. Kumbe wanapewa posho ya 10,000 kweli? wakati wabunge wanajilalia tu bungeni wanapewa 350,000 kwa nini lakini? Haiwezekani kabisa na inasikitisha sana madktari wanafanya kazi kubwa kuliko hao wanaoenda kukoroma bungeni..for real wanafanya kitu gani cha maana...Kwa mtu ambaye ana utu na kufikiria wanadamu wenzake wanaokufa kwa kukosa huduma za afya hospitalini; asingewaongeza wabunge posho. Instead, angewapa madaktari japo kidogo ili warudi kutoa huduma. Tumnajua kuwa hamjali kwa kuwa nyie wenzetu mkijikwaa kidogo mnapanda ndege kwenda nje ya nchi kutibiwa. Ila sisi watoto wa maskini hata Muhimbili kulipaa fees za kumuona huyo daktari shida.... Kwa mtu mwenye akili timamu angepima lipi lina uzito kuwapa posho wakaa bure au kuwaongeza wachapa kazi wanaokoa maisha ya wanyonge...
KIKWETE NA BARAZA LAKE HAWANA UTU...