Friday, May 4, 2012
KWELI ANA MENGI YA KUJIFUNZA
Hivi SHY ROSE alishindwa kutengeneza keki isiyo na rangi zinazohusiana na chama chake? Wakati anajua kabisa anakwenda shrehekea na watu wanaotofautiana kiitikadi. Pichani Mbunge wa CHADEMA Halima Mdee akiikataa keki hiyo...
Picha na Mroki Mroki
Saturday, April 28, 2012
Thursday, April 26, 2012
WAPI USTAARABU WA MWANAMKE?
Zamani nilikuwa nahusisha kutokuwa mstaarabu inatokana na kutokuwa na elimu. Na kuwa wanawake wanaopenda kutumia lugha chafu ni wale ambao hawajasoma. Kumbe nilikuwa najidanganya; kwani siku hizi utaona matusi yanaandikwa mitandaoni mpaka unajiuliza hivi hawa wana akili timamu au wagonjwa? Kusema kweli sielewi kwanini watu tunagombana mitandaoni haswa wanawake na kuandikiana matusi ya nguoni. Tena basi wanawake haohao wanadai kuwa wao ni wasomi really? Msomi hatukani hovyo wala hana muda wa kuandika matusi mitandaoni...Tujirekebishe basi kidogo na kuacha ujinga huo!!!!!
KUNA UMUHIMU WOWOTE WA MUUNGANO?
Kila April 26 ya mwaka tunasherehekea Muungano wa Tanganyika na Zanzibar chini ya hayati JK Nyerere na Abeid Aman Karume. Hivi bado tunauhitaji au ndo wakati umefika wa kuuachia? Wenzetu wazanzibari wanalia kila siku eti wanataka kuwa huru kutoka kwa "wadanganyika" wanavyodai kuwa wananyanyasika sana! Mhh mie sielewi wananyanyasika kivipi. Is it economically, socially or politically? Na kwanini sie watu wa bara tunang'ang'ania muungano? Kuna kitu chochote cha muhimu huko visiwani ambacho tunategemea sana kiasi ambacho tukivunja muungano tutaathirika? Mimi sioni manyanyaso yoyote tunayowapa wazanzibari kama wanavyodai wao. Ninachoona ni faida kubwa tu wanapata kupitia bara.
Subscribe to:
Posts (Atom)

